katika somo hili kuna mambo ambayo huzingatiwa , na kila mwanafunzi ana paswa kuelewqa haya, kwa kuwa Mwishoni mwa moduli hii kila mwanafunzi atakuwa na uwezo wa:
- Kuelewa na kueleza uhusiano uliyopo baina ya lugha na jamii ;
- Kuelewa na kueleza mambo yanayoathiri matumizi ya lugha kwa binadamu ;
- Kubainisha dhana mbalimbali katika isimujamii na kuzihusisha na jamii ya Wanyarwanda ;
- Kufafanua Utendakazi wa dhana za isimujamii katika nyanja za kiisimu na zile za kiisimujamii ;
- Kuchanganua malengo ya isimujamii katika nyanja za lugha na jamii ;
- Kueleza taaluma zenye uhusiano wa karibu na isimujamii;
- Kufafanua na kuchunguza uhusiano wa moja wa isimujamii na taaluma nyinginezo ;
- Kufahamu dhana za sera na upangaji lugha ;
- Kufafanua hatua zinazopitiwa kwa ajili ya kusanifisha na kusambaza istilahi pamoja na asasi zinazoshughulkia kazi hizo ;
- Kueleza maana ya kamusi pamoja na Kubainisha aina mbalimbali za kamusi na kutumia vigezo mbalimbali vya kuainisha msamiati wa kamusi